0:00
0:00

Mlango 7

Ikawa, hapo ukuta ulipojengwa, na milango nimekwisha kuisimamisha, na mabawabu, na waimbaji, na Walawi, wamewekwa,
2 ndipo nilimwagiza ndugu yangu, Hanani, pamoja na yule Hanania, jemadari wa ngome, kuwa na amri juu ya Yerusalemu; kwa maana alikuwa mtu mwaminifu huyo, na mwenye kumcha Mungu kuliko wengi.
3 Nikawaambia, Yasifunguliwe malango ya Yerusalemu kabla halijachomoza jua; nao walinzi wangali wakisimama bado, waifunge milango, mkaikaze; kisha wekeni walinzi wa zamu wa hao wakaao Yerusalemu, kila mtu na zamu yake, na kila mtu kuielekea nyumba yake.
4 Basi mji ulikuwa wa nafasi nyingi, tena mkubwa; lakini watu waliomo walikuwa haba, wala nyumba hazijajengwa.
5 Mungu wangu akanitia moyoni mwangu, kwamba niwakusanye wakuu na mashehe, na watu, ili wahesabiwe kwa nasaba. Nikakiona kitabu cha vizazi vya hao waliokwea hapo kwanza, nikaona ya kwamba imeandikwa humo;
6 Hawa ndio wana wa wilaya, waliokwea kutoka katika ule uhamisho wa hao waliokuwa wamechukuliwa, ambao Nebukadreza, mfalme wa Babeli ,aliwachukua mateka,nao wakarudiYerusalemu na Yuda,kila mtu mjini kwake.
7 ndio hawa waliokuja pamoja na Zerubabeli, Yoshua, Nehemia, Seraya, Reelaya, Nahamani, Mordekai, Bilshani, Mispari, Bigwai, Rehumu, na Baana. Hii ndiyo hesabu ya wanaume wa watu wa Israeli;
8 Wana wa Paroshi, elfu mbili mia moja sabini na wawili.
9 Wana wa Shefatia, mia tatu sabini na wawili.
10 Wana wa Ara mia sita hamsini na wawili.
11 Wana wa Pahath-Moabu, wa wana wa Yeshua na Yoabu, elfu mbili mia nane na kumi na wanane.
12 Wana wa Elamu, elfu moja mia mbili hamsini na wanne.
13 Wana wa Zatu, mia nane arobaini na watano.
14 Wana wa Zakai, mia saba na sitini.
15 Wana wa Binui, mia sita arobaini na wanane.
16 Wana wa Bebai, mia sita ishirini na wanane.
17 Wana wa Azgadi, elfu mbili mia tatu ishirini na wawili.
18 Wana wa Adonikamu, mia sita sitini na saba.
19 Wana wa Bigwai, elfu mbili sitini na saba.
20 Wana wa Adini, mia sita hamsini na watano.
21 Wana wa Ateri, wa Hezekia, tisini na wanane.
22 Wana wa Hashumu, mia tatu ishirini na wanane.
23 Wana wa Besai, mia tatu ishirini na wanne.
24 Wana wa Harifu, mia moja na kumi na wawili.
25 Wana wa Gibeoni, tisini na watano.
26 Watu wa Bethlehemu na Netofa, mia na themanini na wanane.
27 Watu wa Anathothi, mia na ishirini na wanane.
28 Watu wa Beth-Azmawethi, arobaini na wawili.
29 Watu wa Kiriath-Yearimu, na Kefira, na Beerothi, mia saba arobaini na watatu.
30 Watu wa Rama na Geba, mia sita na ishirini na mmoja.
31 Watu wa Mikmashi, mia moja na ishirini na wawili.
32 Watu wa Betheli na Ai, mia moja ishirini na watatu.
33 Watu wa Nebo, hamsini na wawili.
34 Wana wa Elamu wa pili, elfu moja mia mbili hamsini na wanne.
35 Wana wa Harimu, mia tatu na ishirini.
36 Wana wa Yeriko, mia tatu arobaini na watano.
37 Wana wa Lodi, na Hadidi, na Ono, mia saba ishirini na mmoja.
38 Watu wa Senaa, elfu tatu mia kenda na thelathini.
39 Makuhani; Wana wa Yedaya, wa mbari ya Yeshua, mia kenda sabini na watatu.
40 Wana wa Imeri, elfu moja hamsini na wawili.
41 Wana wa Pashuri, elfu moja mia mbili arobaini na saba.
42 Wana wa Harimu, elfu moja na kumi na saba.
43 Walawi; Wana wa Yeshua, wa Kadmieli wa wana wa Hodavia, sabini na wanne.
44 Waimbaji; Wana wa Asafu, mia moja arobaini na wanane.
45 Mabawabu; Wana wa Shalumu, wana wa Ateri, wana wa Talmoni, wana wa Akubu, wana wa Hatita, wana wa Shobai, mia moja thelathini na wanane.
46 Wanethini; wana wa Siha, wana wa Hasufa, wana wa Tabaothi;
47 wana wa Kerosi, wana wa Siaha, wana wa Padoni;
48 wana wa Lebana, wana wa Hagaba, wana wa Salmai;
49 wana wa Hanani, wana wa Gideli, wana wa Gahari;
50 wana wa Reaya, wana wa Resini, wana wa Nekoda;
51 wana wa Gazamu, wana wa Uza, wana wa Pasea;
52 wana wa Besai wana wa Meunimu, wana wa Nefusimu;
53 wana wa Bakbuki, wana wa Hakufa, wana wa Harhuri;
54 wana wa Basluthi, wana wa Mehida, wana wa Harsha;
55 wana wa Barkosi, wana wa Sisera, wana wa Tema;
56 wana wa Nesia, wana wa Hatifa.
57 Akina watumwa wa Sulemani; Wana wa Sotai, wana wa Soferethi, wana wa Peruda;
58 wana wa Yaala, wana wa Darkoni, wana wa Gideli;
59 wana wa Shefatia, wana wa Hatili, wana wa Pokereth-Sebaimu, wana wa Amoni.
60 Wanethini wote, pamoja na akina watumwa wa Sulemani, walikuwa mia tatu tisini na wawili.
61 Na hawa ndio watu waliokwea kutoka Tel-mela, na Tel-harsha, na Kerubu, na Adani, na Imeri; walakini hawakuweza kuonyesha mbari za baba zao, wala kizazi chao, kwamba walikuwa wa Israeli;
62 Wana wa Delaya, wana wa Tobia, wana wa Nekoda, mia sita na arobaini na wawili.
63 Tena katika makuhani; Wana wa Habaya, wana wa Hakosi, wana wa Barzilai, yule aliyeoa mmojawapo binti Barzilai, Mgileadi, akaitwa kwa jina lao.
64 Hao waliitafuta orodha yao miongoni mwa wale waliohesabiwa kwa nasaba, wasionekane; kwa hiyo walihesabiwa kuwa na unajisi.
65 Na huyo Tirshatha akawaambia kwamba wasile katika vile vitu vitakatifu sana, hata atakaposimama kuhani mwenye Urimu na Thumimu.
66 Basi hilo kusanyiko lote zima, jumla yake ilikuwa watu arobaini na mbili elfu na mia tatu na sitini,
67 tena zaidi ya hao, kulikuwa na watumishi wao waume kwa wake, ambao walikuwa elfu saba na mia tatu na thelathini na saba; kisha walikuwa na waimbaji waume kwa wake mia mbili arobaini na watano.
68 Farasi zao walikuwa mia saba thelathini na sita; nyumbu zao, mia mbili arobaini na watano;
69 ngamia zao, mia nne thelathini na watano; punda zao, elfu sita na mia saba na ishirini.
70 Na baadhi ya wakuu wa mbari za mababa walitoa mali kwa ajili ya kazi hii. Yule Tirshatha akatoa kwa ajili ya hazina darkoni za dhahabu elfu moja ,na mabakuli hamsini , na mavazi ya makuhani mia tano na thelathini.
71 Na baadhi ya wakuu wa mbari za mababa wakatoa, na kutia katika hazina ya kazi hiyo, darkoni za dhahabu ishirini elfu, na mane za fedha elfu mbili na mia mbili.
72 Na mabaki ya watu wakatoa darkoni za dhahabu ishirini elfu, na mane za fedha elfu mbili, na mavazi ya makuhani sitini na saba.
73 Hivyo makuhani, na Walawi, na mabawabu, na waimbaji, na baadhi ya watu, na Wanethini, na Israeli wote, wakakaa mijini mwao. Hata ulipowadia mwezi wa saba, wana wa Islaeli walikuwa wakikaa katika miji yao.