0:00
0:00

Mlango 129

Mara nyingi wamenitesa tangu ujana wangu, Israeli na aseme sasa,
2 Mara nyingi wamenitesa tangu ujana wangu, Lakini hawakuniweza.
3 Wakulima wamelima mgongoni mwangu, Wamefanya mirefu mifuo yao.
4 Bwana ndiye mwenye haki, Amezikata kamba zao wasio haki.
5 Na waaibishwe, warudishwe nyuma, Wote wanaoichukia Sayuni.
6 Na wawe kama majani ya darini Yanyaukayo kabla hayajamea.
7 Ambayo mvunaji haujazi mkono wake, Wala mfunga miganda kifua chake.
8 Wala hawasemi wapitao, Amani ya Bwana ikae nanyi, Twawabariki kwa jina la Bwana.