0:00
0:00

Mlango 3

Bwana, watesi wangu wamezidi kuwa wengi, Ni wengi wanaonishambulia,
2 Ni wengi wanaoiambia nafsi yangu, Hana wokovu huyu kwa Mungu.
3 Na Wewe, Bwana, U ngao yangu pande zote, Utukufu wangu na mwinua kichwa changu.
4 Kwa sauti yangu namwita Bwana Naye aniitikia toka mlima wake mtakatifu.
5 Nalijilaza nikalala usingizi, nikaamka, Kwa kuwa Bwana ananitegemeza.
6 Sitayaogopa makumi elfu ya watu, Waliojipanga juu yangu pande zote.
7 Bwana, uinuke, Mungu wangu, uniokoe, Maana umewapiga taya adui zangu wote; Umewavunja meno wasio haki.
8 Wokovu una Bwana; Baraka yako na iwe juu ya watu wako.