0:00
0:00

Mlango 1

Adamu, na Sethi, na Enoshi;
2 na Kenani, na Mahalaleli, na Yaredi;
3 na Henoko, na Methusela, na Lameki;
4 na Nuhu, na Shemu, na Hamu, na Yafethi.
5 Wana wa Yafethi; Gomeri, na Magogu, na Madai, na Yavani, na Tubali, na Mesheki, na Tirasi.
6 Na wana wa Gomeri; Ashkenazi, na Rifathi, na Togama.
7 Na wana wa Yavani; Elisha, na Tarshishi, na Kitimu, na Warodani.
8 Wana wa Hamu; Kushi, na Misri, na Putu, na Kanaani.
9 Na wana wa Kushi; Seba, na Havila, na Sabta, na Raama, na Sabteka. Na wana wa Raama; Sheba, na Dedani.
10 Kushi naye akamzaa Nimrodi; yeye akaanza kuwa mtu hodari katika nchi.
11 Na Misri akazaa Waludi, na Waanami, na Walehabi, na Wanaftuhi,
12 na Wapathrusi, na Wakasluhi; huko ndiko walikotoka Wafilisti, na Wakaftori.
13 Na Kanaani akamzaa Sidoni, mwanawe wa kwanza, na Hethi;
14 na Myebusi, na Mwamori, na Mgirgashi;
15 na Mhivi, na Mwarki, na Msini;
16 na Mwarvadi, na Msemari, na Mhamathi.
17 Wana wa Shemu; Elamu, na Ashuru, na Arfaksadi, na Ludi, na Aramu, na Usi, na Huli, na Getheri, na Mashi.
18 Na Arfaksadi akamzaa Sala, na Sala akamzaa Eberi.
19 Na Eberi akazaliwa wana wawili wa kiume; jina la wa kwanza aliitwa Pelegi, maana katika siku zake nchi iligawanyika; na jina la nduguye aliitwa Yoktani.
20 Na Yoktani akamzaa Almodadi, na Shelefu, na Hasarmawethi, na Yera;
21 na Hadoramu, na Uzali, na Dikla;
22 na Obali, na Abimaeli, na Sheba;
23 na Ofiri, na Havila, na Yobabu. Hao wote ndio wana wa Yoktani.
24 Shemu, na Arfaksadi, na Sala;
25 na Eberi, na Pelegi, na Reu;
26 na Serugi, na Nahori, na Tera;
27 na Abramu, naye ndiye Ibrahimu.
28 Wana wa Ibrahimu; Isaka, na Ishmaeli.
29 Hivi ndivyo vizazi vyao; mzaliwa wa kwanza wa Ishmaeli, Nebayothi; kisha Kedari, na Abdeeli, na Mibsamu;
30 na Mishma, na Duma, na Masa, na Hadadi, na Tema;
31 na Yeturi, na, Nafishi, na Kedema. Hao ndio wana wa Ishmaeli.
32 Na wana wa Ketura, suria yake Ibrahimu; yeye akamzaa Zimrani, na Yokshani, na Medani, na Midiani, na Ishbaki, na Shua. Na wana wa Yokshani; Sheba na Dedani.
33 Na wana wa Midiani; Efa, na Eferi, na Hanoki, na Abida, na Eldaa. Hao wote ndio wana wa Ketura.
34 Na Ibrahimu naye akamzaa Isaka. Wana wa Isaka; Esau, na Israeli.
35 Wana wa Esau; Elifazi, na Reueli, na Yeushi, na Yalamu, na Kora.
36 Wana wa Elifazi; Temani, na Omari, na Sefo, na Gatamu, na Kenazi, na, kwa Timna, Amaleki.
37 Wana wa Reueli; Nahathi, na Zera, na Shama, na Miza.
38 Na wana wa Seiri; Lotani, na Shobali, na Sibeoni, na Ana, na Dishoni, na Eseri, na Dishani.
39 Na wana wa Lotani; Hori, na Hemamu; na Timna ni umbu lake Lotani.
40 Wana wa Shobali; Alvani, na Manahathi, na Ebali, na Shefo, na Onamu. Na wana wa Sibeoni; Aya, na Ana.
41 Wana wa Ana; Dishoni. Na wana wa Dishoni; Hemdani, na Eshbani, na Ithrani, na Kerani.
42 Wana wa Eseri; Bilhani, na Zaawani, na Akani. Wana wa Dishani; Usi, na Arani.
43 Basi hawa ndio wafalme waliomiliki katika nchi ya Edomu, kabla hajamiliki mfalme awaye yote juu ya wana wa Israeli; Bela, mwana wa Beori; na jina la mji wake ni Dinhaba.
44 Bela akafa, naye Yobabu, mwana wa Zera, wa Bosra, akamiliki badala yake.
45 Yobabu akafa, naye Hushamu, wa nchi ya Watemani, akamiliki badala yake.
46 Hushamu akafa, naye Hadadi, mwana wa Bedadi, akamiliki badala yake, ambaye aliwapiga Midiani katika uwanja wa Moabu; na jina la mji wake ni Avithi.
47 Hadadi akafa, naye Samla, wa Masreka, akamiliki badala yake.
48 Samla akafa, naye Shauli, wa Rehobothi karibu na Mto, akamiliki badala yake.
49 Shauli akafa, naye Baal-Hanani, mwana wa Akbori, akamiliki badala yake.
50 Baal-Hanani akafa, naye Hadadi akamiliki badala yake; na jina la mji wake ni Pau; na jina la mkewe ni Mehetabeli, binti Matredi, binti Mezahabu.
51 Akafa Hadadi. Na hawa ndio majumbe wa Edomu; jumbe Timna, na jumbe Alva, na jumbe Yethethi;
52 na jumbe Oholibama, na jumbe Ela, na jumbe Pinoni;
53 na jumbe Kenazi, na jumbe Temani, na jumbe Mibsari;
54 na jumbe Magdieli, na jumbe Iramu. Hao ndio majumbe wa Edomu.