0:00
0:00

Mlango 25

Tena Daudi na maakida wa jeshi wakatenga kwa utumishi baadhi ya wana wa Asafu, na wa Hemani, na wa Yeduthuni, watakaotabiri kwa vinubi na vinanda, na matoazi; hii ndiyo hesabu ya wafanya kazi sawasawa na utumishi wao;
2 wa wana wa Asafu; Zakuri, na Yusufu, na Nethania, na Asharela, wana wa Asafu; walioamriwa na Asafu, aliyetabiri kwa amri ya mfalme.
3 Wa Yeduthuni; wana wa Yeduthuni; Gedalia, na Seri, na Yeshaya, na Hashabia, na Matithia, [na Shimei], watu sita; walioamriwa na baba yao Yeduthuni mwenye kinubi, aliyetabiri katika kumshukuru na kumsifu Bwana.
4 Wa Hemani; wana wa Hemani; Bukia, Matania, Uzieli, Shebueli, na Yeremothi, Hanania, Hanani, Eliatha, Gidalti, na Romanti-ezeri, Yoshbekasha, Malothi, Hothiri, Mahaziothi;
5 hao wote ndio wana wa Hemani, mwonaji wa mfalme, kwa maneno ya Mungu, ili kuinua pembe. Naye Mungu akampa Hemani wana kumi na wanne na binti watatu.
6 Hao wote waliamriwa na baba yao, waimbe nyumbani mwa Bwana, wakiwa na matoazi, vinanda, na vinubi, kwa utumishi wa nyumba ya Mungu; Asafu, Yeduthuni, na Hemani wakiwa wanaamriwa na mfalme.
7 Na hesabu yao, pamoja na ndugu zao waliofundishwa kumwimbia Bwana, wote waliokuwa wastadi, walikuwa mia mbili na themanini na wanane.
8 Wakatupiwa kura ya ulinzi wao, sawasawa wote, mdogo kwa mkubwa, mwalimu kwa mwanafunzi.
9 Kura ya kwanza ikamtokea Yusufu, kwa Asafu; ya pili Gedalia; yeye na nduguze na wanawe, kumi na wawili;
10 ya tatu Zakuri, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
11 ya nne Seri, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
12 ya tano Nethania, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
13 ya sita Bukia, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
14 ya saba Asharela, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
15 ya nane Yeshaya, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
16 ya kenda Matania wanawe na nduguze, kumi na wawili;
17 ya kumi Shimei, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
18 ya kumi na moja Uzieli, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
19 ya kumi na mbili Hashabia, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
20 ya kumi na tatu Shebueli, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
21 ya kumi na nne Matithia, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
22 ya kumi na tano Yeremothi, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
23 ya kumi na sita Hanania, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
24 ya kumi na saba Yoshbekasha, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
25 ya kumi na nane Hanani, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
26 ya kumi na kenda Malothi, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
27 ya ishirini Eliatha, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
28 ya ishirini na moja Hothiri, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
29 ya ishirini na mbili Gidalti, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
30 ya ishirini na tatu Mahaziothi, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
31 ya ishirini na nne Romanti-ezeri, wanawe na nduguze, kumi na wawili.